Na Fedrick Mbaruku - Rukwa
Kama
ilivyo Shirika ni mkono wa pili wa serikali katika kufikia malengo kutokana na
ushirikiano unaofanyika dhidi ya serikali na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali
likiwemo shirika la ADEACH, zaidi ya Wakulima 80 wamepatiwa mafunzo ya kilimo
ikolojia lengo likiwa ni kupambana na udumavu kwa kwa watoto wenze umri chini
za miaka mitano.
Mafunzo
hayo yametolewa Julai 1 mwaka huu katika kata ya Kasense iliyopo Manispaa ya
Sumbawanga Mkoani Rukwa kupitia Shirika la uwezeshaji Tanzania (SAT) kutoka
Mkoani Morogoro kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya Kilimo na Afya ya
Jamii (ADEACH) lililopo Mkoani Rukwa.
Katika
mafunzo hayo ya siku mbili yamewakutanisha wananchi na wadau mbalimbali wa
kulimo ambapo pamoja na mambo mengine wamefundishwa namna ya utengenezaji wa
mbolea, dawa ya kuua wadudu kwenye mimea isiyotumia kemikali ambapo ulaji wa
vyakula vinavyo yalishwa kwa kutumia dawa na viuatilifu vingine kunatajwa kama
sababu mojawapo ya udumavu.
Katika
hatua nyingine wananchi hao wamepewa elimu juu ya kukabiliana na vitendo vya
ukatili kwa watoto vinavyoendelea katika maeneo mbalimbali nchini kwa
kuhakikisha wayayi na waleyi wanakuwa karibu na familia yao.
Mwezeshaji kutoka shirika la uweyeshaji Tanzania (SAT) Rashidi Raswiu amewapongeya wananchi hao kwa kushiriki mafunzo hayo na kuwataka kuzingatia waliyofundishwa na wataalam huku akisema kutokana na mwitikio wao SAT iataweka nguvu kwa wakulima wa Mkoa wa Rukwa ili kuwasaidia kufikia malengo yao.
















Tunapatikana Kupitia