Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia Kikao cha Umoja wa Afrika (AU) kuhusu masuala ya G20, katika Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU), uliofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia, tarehe 14 Februari, 2026.

Rais Dkt. Samia aliwasilisha msimamo wa Tanzania kuhusu vipaumbele vya maendeleo, ikiwemo kuimarisha matumizi ya nishati safi, usimamizi wa madeni ya nchi, ustahimilivu dhidi ya majanga ya tabianchi, uongezaji thamani wa rasilimali za madini, pamoja na kuimarisha usalama wa chakula.
#MaendeleoEndelevu 
#DiplomasiaYaKiuchumi
#KaziNaUtuTunasongaMbele