Kamishina mkuu wa mamlaka ya mapato tanzaniaTRA Bwa. Yusuph Juma Mwenda amewashukuru na kuwapongeza wafanza biashara wa mkoa wa Rukwa kwa ulipaji kodi wa hiari hali iliyo changia mkoa kuvuka lengo la kukusanya kodi kwa asilimia 130 kwa mwaka wa fedha ulioisha 2024/2025.
Mwenda amesema hayo katika kiko kilicho wakutanisha
wafanya biashara wa mkoa wa Rukwa na kamishina mkuu huyo kilicho fanyika jana
tarehe 3 Julai,2025 katika ukumbi mkubwa wa mikutano uliopo ofisi ya mkuu wa
mkoa wa Rukwa.
Mbali na pongezi hizo Mwenda amewahakikishia wazabuni na
wakandarasi wanaoidai serikali kuwa watalipwa madeni.
“Lazima madeni yenu ya ndani yalipwe na mimi nitakuwa
balozi wenu hasa kwa wale wanaotudai kuwasema zaidi wale wenye madeni na justification uwenda
yapo wizara ya fedha,au yapo wizara mbalimbali kama ujenzi ili muendelee kulipa
kodi sisi kama TRA tutakuwa mabalozi wenu kuwasemea,” kamishina mkuu TRA
Tunapatikana Kupitia