Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa
CHADEMA, Brenda Rupia amemshukia Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Stephen Wasira,
akipinga kauli yake kuwa hakuna kesi za kisiasa nchini.
Akizungumza na wanahabari leo, Jumamosi, Februari 21, 2026, Mkurugenzi huyo
amemtaka Wasira kueleza ni jina gani lingine linaweza kupewa kesi ya uhaini
inayomkabili Tundu Lissu, ambayo imemfanya akae gerezani kwa siku 319 sasa.
CHADEMA inadai kuwa kesi hiyo imetengenezwa ili kumpa "ahueni"
mgombea wa CCM dhidi ya upinzani na kwamba mchakato huo ni matumizi mabaya ya
rasilimali za nchi.

“Wewe kesi kama hiyo wewe unaiitaje? Maana mimi sielewi ukisema hizi kesi sio
za kisiasa, hii kesi wewe unaiitaje? Mwenyekiti anakaa gerezani sio kwa kupenda
anapotezewa muda, hakuna njia nyingine ya kuisema.
Mnampotezea mwenyekiti muda,
mnawapotezea wanachama wa CHADEMA muda kwa kila siku kwenda mahakamani
kushuhudia kesi ya uongo”, ameeleza Rupia.


Tunapatikana Kupitia