Mkuu wa
Wilaya ya Sumbawanga Mhe. Nyakia Ally Chirukile amesisitiza umuhimu kwa
jamii kuzingatia matumizi sahihi ya chakula chenye makundi yote ya lishe
ili kuhakikisha afya bora na kuepuka tatizo la udumavu katika jamii.
Mhe.
Chirukile amesema ni muhimu kwa Wananchi kutumia mazao wanayolima kwa
kuzingatia mlo kamili, badala ya kujikita katika aina moja ya chakula,
ili kuimarisha afya za watoto katika ngazi ya kaya na jamii kwa ujumla.
Wito
huo ameutoa leo Februari 20, 2026, wakati akizungumza katika kikao cha
tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa Halmashauri ya Manispaa
ya Sumbawanga, Robo ya Pili 2025/2026.
Aidha, amesisitiza kuwa
lishe bora ni msingi wa maendeleo ya jamii hivyo ni wajibu wa kila
mwananchi kuhakikisha anatumia vyakula vyenye makundi yote ya chakula
ili kujenga jamii yenye afya na nguvu kazi imara.
Tunapatikana Kupitia