Malumbano hayo yametokana na notisi iliyowasilishwa na Jamhuri mahakamani ya kuongeza ushahidi mpya kwa mmoja wa mashahidi wake, unaotokana na upelelezi wa matukio ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ambayo Lissu ameipinga vikali kuwa si halali na kwamba itaibua matatizo makubwa.
Leo, Jumatatu, Februari 23, 2026, upande wa mashtaka umeieleza Mahakama kuwa Februari 18, 2026 uliwasilisha mahakamani kwa njia ya mtandao notisi ya kuongeza ushahidi katika kesi hiyo.
Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, amesema Jamhuri imewasilisha notisi hiyo kwa mujibu wa kifungu cha 308(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), Marejeo ya mwaka 2023.
Katuga amesema katika notisi hiyo hawaombi kuongeza shahidi mpya, bali ushahidi mpya katika ushahidi wa shahidi, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Amin Mahamba, na kwamba wameambatanisha kiini cha ushahidi huo mpya.
Akijibu hoja za Wakili Katuga, Lissu amesisitiza kuwa kifungu cha 308 cha CPA kinazungumzia shahidi mpya, na si ushahidi mpya wa shahidi, shahidi mpya ni yule ambaye maelezo yake au ushahidi wake haukusomwa kwenye mwenendo kabidhi.

Tunapatikana Kupitia